Koloseo
Koloseo ilijengwa kuanzia mwaka 70 hadi 80 BK. Kaisari Vespasiano alianzisha ujenzi kwa kutumia mapato ya uwindo wa vita ya Waroma dhidi ya Uyahudi na hasa hazina ya hekalu ya Yerusalemu. Ilikamilishwa na Kaisari Titus.
Kiwanja kilikuwa na nafasi kwa watu 45,000 hadi 50,000. Watazamaji waliangalia maonyesho ambako watu au wanyama waliuawa. Michezo hii iligharamiwa na serikali kwa ajili ya wakazi wa mji kama burudani. Falsafa ya kisiasa ya Roma ilisema ya kwamba watu watulia wakipewa "panem et circenses" yaani "chakula na michezo".
Baada ya ushindi wa Ukristo mashindano ya kuua watu yalipingwa na kanisa. Shindano la mwisho lilitokea mwaka 434/435. Mapigano dhidi ya wanyama yaliendelea hadi mwaka 523. Lakini baada ya mwisho wa Dola la Roma idadi ya wakazi wa Roma ilipungua na Koloseo haikutumiwa tena kwa michezo.
Katika karne zilizofuata wakazi wa Roma walitumia Koloseo kama windo la mawe kwa ajiliy a ujenzi. Hivyo sehemu kubwa ya jengo imepotea.
Michezo katika Koloseo
Michezo katika Koloseo ilikuwa hasa ya aina mbili:- mashindano ya wapiganaji walioshindana kwa silaha za kweli hadi kifo. Wapiganaji waliitwa na Waroma kwa jina la "gladiator" yaani mwenye upanga. Wengi wao walikuwa watumwa lakini wengine walikuwa watu huru. Walijifunza mapigano kwa silaha kwa ajili ya maonyesho na kuitumia kwenye kiwanja mbele wa watazamaji. Walioshinda walipata tuzo na zawadi nyingi. Wegine walikufa na kusahauliwa.
- mashindano kati ya watu na wanyama pori. Waroma wa Kale walikamata wanyama pori kutoka Ulaya na Afrika ya KAskazini kwa ajili ya maonyesho haya. Wanyama waliuawa kwenye kiwanja mbele ya watazamaji na magladiator lakini ilitokea pia ya kwamba wavindaji waliuawa na wanyama.
- kiwanja kilijazwa maji na jahazi pia manowari ndogo ziliwekwa humo ili zishindane. Michezo hii ilikuwa ghali sana na ni makaisari tu walioweza kugharamia michezo ya aina hii.
- Tangi karne ya 3 Wakristo waliuawa kiwanjani kama sehemu ya maonyesho. Ukristo ulikuwa dini marufuku katika Roma ya Kale hadi mwaka 313. Wakati mwingine Wakristo walikamtawa kwa wingi na kupewa hukumu ya mauti. Walionekana walifaa kwa maonyesho ambako walisimamishwa mbele ya wanyama pori kama simba au dubu.
No comments:
Post a Comment