Monday 30 July 2018
Wazimbabwe wapiga kura katika uchaguzi wa kihistoria
Wazimbabwe wapiga kura katika uchaguzi wa kihistoria
Wazimbabwe wanapiga kura katika uchaguzi wao wa kwanza
bila jina la Robert Mugabe kuwa kwenye karatasi za kupigia kura. Ni
uchaguzi ambao huenda ukaifanya nchi hiyo kutambuliwa zaidi kimataifa na
kuimarisha uwekezaji
Karibu watu milioni 5.5 wamesajiliwa kupiga kura katika taifa hilo la
Kusini mwa Afrika ambalo lina shauku kubwa ya kuona mabadiliko baada ya
mkwamo wa kiuchumi na kisiasa wakati wa utawala wa karibu miongo minne
wa Mugabe mwenye umri wa miaka 94. Maelfu ya waangalizi wa uchaguzi
wamesambazwa kote nchini humo kuuangalia mchakato huo ambao upinzani
unasema unaupendelea upande wa serikali licha ya kuhakikishiwa na tume
ya uchaguzi kuwa utakuwa wa kuaminika.
Wagombea wawili wakuu ni Rais Emmerson Mnangagwa mwenye umri wa miaka 75, na ambaye alikuwa makamu wa rais aliyechukua usukani baada ya Mugabe kujiuzulu chini ya shinikizo la kijeshi mwaka jana, na Nelson Chamisa mwenye umri wa miaka 40, wakili na mhubiri ambaye alichukua uongozi wa chama kikuu cha upinzani Movevement for Democratic Change – MDC miezi michache iliyopita baada ya kifo cha kiongozi wake Morgan Tsvangirai. Tume ya uchaguzi imesema itatoa matokeo baada ya siku tano. Chamisa amepiga kura yake akisema kuwa ana uhakika wa kupata ushindi.
Mnangagwa alidai kuwa matamshi hayo ya Mugabe yalidhihirisha kuwa Chamisa yuko katika muungano na Mugabe. Lakini Chamisa pia alizungumza akisema hana chochote cha kuzungumzia kuhusu kauli ya Mugabe kwa sababu ana haki ya kusema chochote kama mpiga kura. Mnangagwa ambaye anatuhumiwa kwa kuhusika katika machafuko ya uchaguzi na udanganyifu chini ya Mugabe, amewaalika waangalizi wa kimataifa – ikiwemo timu ya Umoja wa Ulaya.
Aliyekuwa rais wa Liberia Ellen Sirleaf Johnson ambaye ni kiongozi wa ujumbe wa uangalizi wa kimataifa amesema huu ni wakati muhimu sana katika safari ya demokrasia ya Zimbabwe. Uwepo wa waangalizi wa uchaguzi kutoka nchi za magharibi kwa mara ya kwanza katika miaka mingi ni kiashiria cha mazingira huru ya kisiasa, ijapokuwa wasiwasi umeibuliwa kuhusu upendeleo wa vyombo vya habari vya serikali kwa chama tawala cha Zanu PF pamoja na ukosefu wa uwazi katika uchapishaji wa karatasi za kupigia kura.
Serikali ijayo lazima ipambane na ukosefu mkubwa wa ajira na uchumi ulioharibiwa na sera iliyoungwa mkono na Mugabe ya kutwaa mashamba yaliyomilikiwa na wazungu, kuanguka kwa kilimo, kiwango kikubwa cha mfumko wa bei na kuhama kwa wawekezaji.
Mwandishi: rama dee
Mhariri: musa msikiti
Wagombea wawili wakuu ni Rais Emmerson Mnangagwa mwenye umri wa miaka 75, na ambaye alikuwa makamu wa rais aliyechukua usukani baada ya Mugabe kujiuzulu chini ya shinikizo la kijeshi mwaka jana, na Nelson Chamisa mwenye umri wa miaka 40, wakili na mhubiri ambaye alichukua uongozi wa chama kikuu cha upinzani Movevement for Democratic Change – MDC miezi michache iliyopita baada ya kifo cha kiongozi wake Morgan Tsvangirai. Tume ya uchaguzi imesema itatoa matokeo baada ya siku tano. Chamisa amepiga kura yake akisema kuwa ana uhakika wa kupata ushindi.
Zimbabwe inakabiliwa na matatizo ya kiuchumi
Zaidi
ya wagombea 20 na karibu vyama vya kisiasa 130 vinashiriki katika
uchaguzi huo. Kama hakuna mgombea wa urais atakayepata asilimia 50 ya
kura, basi duru ya pili itaandaliwa Septemba 8. Ni uchaguzi wa kwanza
kuandaliwa bila Mugabe aliyekiongoza chama cha ZANU PF kuingia
madarakani katika uchaguzi wakati nchi hiyo ilipopata uhuru kutoka kwa
utawala wa Waingereza mwaka wa 1980 na akaongoza kwa miaka 37.
Akizungumza katika makazi yake mjini Harare jana, Mugabe alisema
anatumai kuwa uchaguzi huo utaiondoa madarakani serikali isiyo ya
kikatiba.Mnangagwa alidai kuwa matamshi hayo ya Mugabe yalidhihirisha kuwa Chamisa yuko katika muungano na Mugabe. Lakini Chamisa pia alizungumza akisema hana chochote cha kuzungumzia kuhusu kauli ya Mugabe kwa sababu ana haki ya kusema chochote kama mpiga kura. Mnangagwa ambaye anatuhumiwa kwa kuhusika katika machafuko ya uchaguzi na udanganyifu chini ya Mugabe, amewaalika waangalizi wa kimataifa – ikiwemo timu ya Umoja wa Ulaya.
Aliyekuwa rais wa Liberia Ellen Sirleaf Johnson ambaye ni kiongozi wa ujumbe wa uangalizi wa kimataifa amesema huu ni wakati muhimu sana katika safari ya demokrasia ya Zimbabwe. Uwepo wa waangalizi wa uchaguzi kutoka nchi za magharibi kwa mara ya kwanza katika miaka mingi ni kiashiria cha mazingira huru ya kisiasa, ijapokuwa wasiwasi umeibuliwa kuhusu upendeleo wa vyombo vya habari vya serikali kwa chama tawala cha Zanu PF pamoja na ukosefu wa uwazi katika uchapishaji wa karatasi za kupigia kura.
Serikali ijayo lazima ipambane na ukosefu mkubwa wa ajira na uchumi ulioharibiwa na sera iliyoungwa mkono na Mugabe ya kutwaa mashamba yaliyomilikiwa na wazungu, kuanguka kwa kilimo, kiwango kikubwa cha mfumko wa bei na kuhama kwa wawekezaji.
Mwandishi: rama dee
Mhariri: musa msikiti
Subscribe to:
Posts (Atom)