Monday 16 April 2018

Watu 257 wafa kwenye ajali ya ndege Algeria

Watu 257 wafa kwenye ajali ya ndege Algeria

Takriban watu 257 waliokuwa kwenye ndege ya kijeshi nchini Algeria wamefariki dunia baada ya ndege hiyo kuanguka nje ya mji mkuu wa nchi hiyo Algiers. Ndege hiyo iliwaka moto baada ya kuanguka.
Militärflugzeug in Algerien abgestürzt (Reuters/R. Boudina)
Takriban watu 257 waliokuwa kwenye ndege ya kijeshi nchini Algeria wamefariki dunia baada ya ndege hiyo kuanguka nje ya mji mkuu wa nchi hiyo Algiers hii leo. Kulingana na shirika la habari la serikali, ndege hiyo iliwaka moto baada ya kuanguka katika tukio linalotajwa kuwa baya zaidi kwenye usafiri wa anga kuwahi kushuhudiwa nchini humo. 
Picha zilizorushwa na kituo kimoja cha televisheni kinaonyesha watu na magari ya msaada wa dharura wakiwa wamefurika kuzunguka eneo hilo la ajali lililotawaliwa na moshi na moto, karibu na uwanja wa ndege wa kijeshi kwenye kambi ya Boufarik kusinimagharibi mwa Algiers. 
Wizara ya ulinzi imesema, jumla ya watu 257 wamekufa, wengi miongoni mwao ni wanajeshi. Wahudumu 10 wa ndege na baadhi ya abiria waliokufa wamekwishatambuliwa na jamaa zao. Imeongeza kuwa manusura kadhaa wanaendelea kupata matibabu katika hospitali ya jeshi, na miili ya wahanga wa ajali hiyo imepelekwa hospitalini hapo kwa ajili ya utambuzi.
Chanzo cha ajali bado hakijajulikana na tayari kumeanzishwa uchunguzi.
Militärflugzeug in Algerien abgestürzt (Reuters/Ennahar Tv)
Ni tukio la kwanza kwa ndege za jeshi la algeria kutokea tangu mwaka 2014.
Mmoja wa wanachama wa chama tawala cha National Liberation Front, FLN, amekiambia kituo binafsi cha televisheni kwamba miongoni mwa waliokufa ni wanachama wa kikundi cha wanaotaka uhuru wa taifa jirani la Sahara Magharibi, la Polisario, linaloungwa mkono na serikali ya Algeria. Eneo hilo la Sahara Magharibi linazozaniwa kwa muda mrefu na Morocco na Algeria. 
Ni miongoni mwa matukio yaliyowahi kutokea, ingawa hili ni baya zaidi.
Ndege hiyo ilikuwa inaelekea katika mji wa Tindouf, ulioko mpakani mwa Algeria na Sahara Magharibi, lakini ilianguka katika eneo la uwanja wa ndege, hii ikiwa ni kulingana na wizara ya ulinzi. Tindouf ni makazi ya maelfu ya wakimbizi na wengi wakitokea Sahara Magharibi, ambao miongoni mwao ni wafuasi wa Polisario.  
Kulingana na kituo cha televisheni cha Dzair, watu watano wako katika hali mbaya. Mkulima mmoja amekiambia kituo cha televisheni cha Ennahar kwamba aliwaona baadhi ya abiria waliruka kutoka kwenye ndege hiyo kabla ya kuanguka. 
Ofisi ya waziri mkuu imesema wabunge walisimama kimya kwa dakika moja kuwaombea wahanga wa ajali hiyo. 
Ndege hiyo chapa 11-76 iliyoundwa nchini Urusi miaka ya 1970 kwa muda wote imekuwa na rekodi nzuri ya kiusalama. Imekuwa ikitumiwa kwa usafirishaji wa mizigo na abiria. 
Tukio hili ni la kwanza kwa ndege za jeshi la Algeria kutokea, tangu lile la mwezi Februari mwaka 2014, ambapo ndege iliyotengenezwa nchini Marekani chapa C-130 Hercules turboprop ilipoanguka kwenye milima ya Algeria, na kusababisha vifo vya watu 76 na mmoja tu alinusurika.
Tukio baya zaidi la ajali ya ndege kutokea kwenye ardhi ya Algeria ni la mwaka 2003, wakati watu 102 walipokufa na mmoja kunusurika baada ya ndege ya kiraia kuanguka ilipofika mwishoni mwa njia ya kurukia katika uwanja wa Tamanrasset. 

Winnie Mandela hatuta msahau

Winnie Mandela apewa mazishi ya kitaifa

Maelfu ya watu wamekusanyika Jumamosi (14.04.2018) katika uwanja wa mpira wa Soweto kutoa heshima zao za mwisho kwa mwanaharakati wa kupinga ubaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini Winnie Madikizela-Mandela.
Südafrika Bebgräbnis von Winnie Madikizela-Mandela in Johannesburg (Reuters/S. Sibeko)
Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa ametoa heshima yake iliyojawa hisia akiahidi kupendekeza Bi. Winnie apokee heshima ya juu ndani ya chama tawala cha African National Congress ANC. Ramaphosa amemtaja Winnie kama mtu aliyekuwa akijivunia, mtetezi na mwenye kueleza kwa ufasaha aliyefichua uongo wa wabaguzi.
Amesema kuwekwa kizuizini, mateso na miaka ya marufuku ambayo Madikizela-Mandela alipitia, vilimtia hamasa kama mwanaharakati wa kisiasa, lakini pia vilisababisha majeraha makubwa ambayo hayajawahi kupona na kwa kiasi kikubwa kupuuzwa na rika nyingi.
Winnie Madikizela-Mandela aliyefariki Aprili 2, akiwa na umri wa miaka 81 amezikwa kwa heshima ya kitaifa ambapo jeneza lake lilibebwa na askari wakati mwili wake ukiingizwa katika uwanja wa Soweto.
Viongozi kadhaa wa nchi walihudhuria mazishi hayo akiwemo rais wa Congo Brazzaville Denis Sassou Nguesso, waziri mkuu wa taifa jirani la Lesotho Pakalitha Mosisili; na wajumbe wengine kutoka serikali za afrika na vyama vya ukombozi. Marais wa zamani wa Afrika Kusini Jacob Zuma na Thabo Mbeki pia nao walihudhuria mazishi ya mpambanaji huyo aliyejulikana mama wa taifa au mama Winnie.
Mwandishi: Radick Nap Africa
Mhariri: Rama Dee

Wanasiasa wa Urusi wakutana na al-Assad

Wanasiasa wa Urusi wakutana na al-Assad

Wanasiasa wa Urusi wamekutana na Rais wa Syria Bashar al-Assad, siku moja baada ya mashambulizi ya pamoja ya angani ya Marekani, Uingereza na Ufaransa nchini Syria
Syrien Regierungstruppen in Ost-Ghouta (Getty Images/AFP/Y. Karwashan)
Vyombo vya habari vya Urusi vimesema Al-Assad ameusifu mfumo wa enzi ya Kisovieti wa kujikinga dhidi ya makombora ambao Syria inaripotiwa kutumia kuyaripua karibu makombora 70 kati ya 100 yaliyofyatuliwa wakati wa mashambulizi hayo.
Pia ameyaelezea mashambulizi hayo kuwa kitendo cha uchokozi wa nchi za Magharibi, maoni ambayo yameungwa mkono na wabunge hao wa Urusi waliomtembelea.
Kwa mujibu wa shirika la habari la Urusi TASS, Sergei Zheleznyak amesema baada ya mkutano na al-Assad kuwa kutokana na mtazamo wa rais, huu ni uchokozi na tunamuunga mkono.
UN-Sicherheitsrat in New York | Abstimmung Syrien (Reuters/E. Munoz)
Baraza la Usalama lilipinga azimio la Urusi
Warusi hao waliomtembelea wamemuelezea al-Assad kuwa katika "hisia nzuri”. Rais huyo wa Syria pia ameripotiwa kukubali mwaliko wa kuitembelea Siberia, ijapokuwa haijafahamika ni lini ziara hiyo itafanyika. Juammosi, rasimu ya azimio lililowasilishwa na Urusi katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa likiyalaani mashambulizi hayo ya angani halikupitishwa.
Kazi ya OPCW yaanza mjini Douma
Ziara ya wanasiasa hao imefanywa katika siku moja ambayo shirika la habari la Ufaransa – AFP limeripoti kuwa wakaguzi kutoka Shirika la Kimataifa la Kudhibiti Matumizi ya Silaha za Sumu – OPCW wanatarajiwa kuanza uchunguzi wao wa kubaini kama silaha za gesi ya klorini au sarin zilitumiwa dhidi ya raia katika shamubulizi hilo la Aprili 7 mjini Douma.
Wapelelezi hao waliwasili Juammosi, muda mfupi tu baada ya mashmbulizi hayo ya washirika kufanywa. Urusi na Iran ambayo ni mshirika wake anayemuunga mkono Syria ziliyalaani mashambulizi hayo ya angani yaliyoongozwa na Marekani kwa kufanywa kabla ya shirika la OPCW kufanya uchunguzi.
Mkutano wa kilele wa Jumuiya ya Kiarabu kuijadili Syria
Kairo Arabische Liga Außenministertreffen Jerusalemfrage (picture-alliance/Photoshot/A. Gomaa)
Jumuiya ya Kiarabu ilikutana mwisho Machi 2017
Wakati Assad aliwaalika wabunge wa Urusi, viongozi wengine wa mataifa ya Kiarau walikutana nchini Saudi Arabia leo Jumapili kwa mkutano wao wa kilele wa kila mwaka wa Jumuiya ya Kiarabu, ambao ulikuwa umeahirishwa mwezi uliopita kutokana na uchaguzi wa Misri.
Karibu wakuu 17 wa mataifa ya Kiarabu walitarajiwa kuhudhuria mkutano huu mjini Dhaharan. Al-Assad hajashiriki katika mkutano huo wa kilele tangu 2011, wakati shirika hilo lenye nchi 22 wanachama lilipoufuta uwanachama wake.
Ujumbe wa Qatar unaongozwa na mwakilishi wake wa kudumu katika Jumuiya ya Kiarabu, badala ya afisa mwandamizi katika ufalme wa nchi hiyo – ishara kuwa mvutano wa kikanda kati ya Qatar na baadhi ya mairani zake bado ni mkubwa.
Miongoni mwa mada kuu zinazotarajiwa kujadiliwa katika mkutano huo wa kilele ni pamoja na kitu kinachoonekana kuwa ni Iran kuingilia masuala ya nchi za Kiarabu, kama vile vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Yemen na katika kuunga mkono mapigano ya Washia nchini Iraq.
Mashambulizi ya angani nchini Syria mwishoni mwa wiki na vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyodumu miaka saba sasa nchini humo pia ni mambo yanayotarajiwa kujadiliwa.
Mwandishi: Radick nap Africa
Mhariri: Rama Dee

Monday 9 April 2018

Zuma awa ngangari mbele ya mashtaka ya rushwa

Zuma awa ngangari mbele ya mashtaka ya rushwa
Rais wa zamani wa Afrika Kusini Jacob Zuma alifikishwa kizimbani katika mahakama iliyofurika Ijumaa kukabili mashtaka ya rushwa na aliibuka mkaidi, akiyataja mashtaka hayo kuwa yaliochochewa kisiasa.
Jacob Zuma Durban Südafrika (picture-alliance/AP/T Hadebe)
Zuma mwenye umri wa miaka 75, alionekana mtulivu wakati wa usikilizaji wa kwanza wa kesi hiyo uliodumu kwa dakika 15 tu, ambapo kesi hiyo iliahirishwa hafi Juni 8.
Jaji Themba Sishi ameahirisha kesi hiyo, baada ya kuwasilikiza mawakili wa pande zote waliothibitisha kuwa Zuma atakata rufaa kupinga uamuzi wa kumshitaki. Polisi iliimarisha usalama nje ya jengo la mahakama, lakini tukio hilo limepita kwa amani.
Wakati mapambano ya muda mrefu yanatarajiwa, tukio la Zuma kusimama mbele ya majaji chini ya miezi mwili baada ya kujiuzulu wadhifa wake, lilikuwa ushindi kwa wanasiasa wa upinzani na wanaharakati waliopigana kwa miaka kadhaa kumuwajibisha.
Mashtaka yanayomkabili Zuma
Mashitaka 16 ya hongo, udanganyifu na utakatishaji fedha yalirejeshwa hivi karibuni baada ya kutupiliwa mbali karibu muongo mmoja uliopita. Yanahusiana na mkataba wa silaha katika miaka ya 1990, wakati Zuma alipokuwa naibu rais.
Südafrika | Präsident Zuma tritt zurück ARCHIV (Reuters/R. Ward)
Wafuasi wa Zuma wanaamini kiongozi wao anaandamwa tu na hana hatia.
Zuma anashtumiwa kwa kuchukuwa hongo kutoka kampuni ya Ufaransa inayotengeneza silaha ya Thales, katika mkataba wa mamilioni ya dola, wakati alipokuwa waziri wa uchumi na wakati huo makamu wa rais wa chama tawala cha Afrika Kusini, ANC.
Kampuni ya Thales, ambayo iliiuzia Afrika Kusini meli za kivita kama sehemu ya mkataba huo, pia inakabiliwa na mashtaka ya rushwa na mwakilishi wa kampuni hiyo alihudhuria mahakamani pamoja na Zuma.
Zuma anadaiwa kuchukuwa kinyume na sheria jumla ya Randi milioni 4.7, sawa na Euro 280,000 kwa kiwango cha sasa cha ubadilishaji fedha -- kutoka malipo 783 yaliyoshughulikiwa na Schabir Shaik, mfanyabiashara aliyekuwa mshauri wake wa kibiashara. Shaik alihukumiwa kifungo cha miaka 15 gerezani mwaka 2005 kwa tuhuma sawa na hizo, lakini uchunguzi uliookolewa sana mwaka 2016, ulimuondolea lawama Zuma.
Zuma ambaye aliingia madarakani mwaka 2009 baada ya kuondolewa mashtaka, anakanusha kutenda kosa lolote, na anadai kuwa tume ya uchunguzi ilithibitisha kuwa hakuna ushahidi wowote kwamba fedha zilizopokelewa na yeyote miongoni mwa washauri zililipwa kwa afisa yeyote.
Adai kuandamwa kisiasa
Nje ya jengo la mahakama, Zuma aliimba na kucheza jukwani mbele ya kundi kubwa la wafuasi wake, wengi wao wakiwa wamevalia nguo za rangi za chama cha ANC. Aliwambia wafuasi kuwa yeye ni mhanga wa visasi vya kisiasa.
Aliongeza kuwa amekuwa akipigania haki za za kiuchumi za raia weusi wa Afrika Kusini walio wengi tangu kumalizika kwa utawala wa kibaguzi wa weupe wachache mwaka 1994.
Ujumbe huo unavuma miongoni mwa watu wengi wanaochukia ukweli kwambasehemu kubwa ya uchumi inaendelea kuwa mikononi mwa wazungu wachache licha ya kuja kwa demokrasia.
Südafrika - neuer Präsident Cyril Ramaphosa (picture-alliance/AP Photo)
Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa ameapa kupambana na rushwa aliokiri kuwa tatizo kubwa kwa taifa hilo.
"Mtu anapotuhumiwa kwa uhalifu, hilo halimaanishi kwamba wamekutwa na hatia. Mtu huyo bado ana haki kama mtu mwingine yeyote," alismea Zuma.
ANC yamtupa mkono
Mwezi uliopita mwendesha mashtaka mkuu wa Afrika Kusini Shaum Abrahams -- aliyepachikwa jina la utani la "Shaun Kondo" -- kutokana na utiifu wake kwa Zuma wakati wa urais wake -- aliagiza Zuma ashitakiwe kwa udanganyifu, rushwa na utakatishaji fedha.
Chama cha ANC kilimlaazimisha Zuma kuachia madaraka mwezi Februari, kutokana kwa sehemu kubwa na changamoto za kisheria zilizokuwa zikiongezeka dhidi yake pamoja na kashfa kadhaa za rushwa, na chama hicho kimejitenga na kiongozi wake huyo wa zamani.
Mrithi wa Zuma Cyril Ramaphosa ameapa kupambana dhidi ya rushwa serikalini, ambayo alikiri kuwa ni tatizo kubwa.
Mwandishi: ramadhani daud
Mhariri: rama dee