Monday 30 July 2018

asili yetu

Vidio zaidi

Königin von Sheba (Comic Republic)

Kutana na Malkia wa Sheba

Bayajida - baba wa kabila la Hausa

Mtambue Dinknesh

Kutana na Mwalimu Julius Nyerere

Illustrationen - African Roots (Comic Republic)

Kutana na Cheikh Diop, mwanasayansi wa Kiafrika

Mjue Kinjekitile Ngwale

Unamfahamu Kwame Nkrumah?

Wazimbabwe wapiga kura katika uchaguzi wa kihistoria


Wazimbabwe wapiga kura katika uchaguzi wa kihistoria

Wazimbabwe wanapiga kura katika uchaguzi wao wa kwanza bila jina la Robert Mugabe kuwa kwenye karatasi za kupigia kura. Ni uchaguzi ambao huenda ukaifanya nchi hiyo kutambuliwa zaidi kimataifa na kuimarisha uwekezaji
Simbabwe Präsidentenwahl (Reuters/M. Hutchings)
Karibu watu milioni 5.5 wamesajiliwa kupiga kura katika taifa hilo la Kusini mwa Afrika ambalo lina shauku kubwa ya kuona mabadiliko baada ya mkwamo wa kiuchumi na kisiasa wakati wa utawala wa karibu miongo minne wa Mugabe mwenye umri wa miaka 94. Maelfu ya waangalizi wa uchaguzi wamesambazwa kote nchini humo kuuangalia mchakato huo ambao upinzani unasema unaupendelea upande wa serikali licha ya kuhakikishiwa na tume ya uchaguzi kuwa utakuwa wa kuaminika.
Wagombea wawili wakuu ni Rais Emmerson Mnangagwa mwenye umri wa miaka 75, na ambaye alikuwa makamu wa rais aliyechukua usukani baada ya Mugabe kujiuzulu chini ya shinikizo la kijeshi mwaka jana, na Nelson Chamisa mwenye umri wa miaka 40, wakili na mhubiri ambaye alichukua uongozi wa chama kikuu cha upinzani Movevement for Democratic Change – MDC miezi michache iliyopita baada ya kifo cha kiongozi wake Morgan Tsvangirai. Tume ya uchaguzi imesema itatoa matokeo baada ya siku tano. Chamisa amepiga kura yake akisema kuwa ana uhakika wa kupata ushindi.
Simbabwe Präsidentenwahl (Reuters/M. Hutchings) Zimbabwe inakabiliwa na matatizo ya kiuchumi
Zaidi ya wagombea 20 na karibu vyama vya kisiasa 130 vinashiriki katika uchaguzi huo. Kama hakuna mgombea wa urais atakayepata asilimia 50 ya kura, basi duru ya pili itaandaliwa Septemba 8. Ni uchaguzi wa kwanza kuandaliwa bila Mugabe aliyekiongoza chama cha ZANU PF kuingia madarakani katika uchaguzi wakati nchi hiyo ilipopata uhuru kutoka kwa utawala wa Waingereza mwaka wa 1980 na akaongoza kwa miaka 37. Akizungumza katika makazi yake mjini Harare jana, Mugabe alisema anatumai kuwa uchaguzi huo utaiondoa madarakani serikali isiyo ya kikatiba.
Mnangagwa alidai kuwa matamshi hayo ya Mugabe yalidhihirisha kuwa Chamisa yuko katika muungano na Mugabe. Lakini Chamisa pia alizungumza akisema hana chochote cha kuzungumzia kuhusu kauli ya Mugabe kwa sababu ana haki ya kusema chochote kama mpiga kura. Mnangagwa ambaye anatuhumiwa kwa kuhusika katika machafuko ya uchaguzi na udanganyifu chini ya Mugabe, amewaalika waangalizi wa kimataifa – ikiwemo timu ya Umoja wa Ulaya.
Aliyekuwa rais wa Liberia Ellen Sirleaf Johnson ambaye ni kiongozi wa ujumbe wa uangalizi wa kimataifa amesema huu ni wakati muhimu sana katika safari ya demokrasia ya Zimbabwe. Uwepo wa waangalizi wa uchaguzi kutoka nchi za magharibi kwa mara ya kwanza katika miaka mingi ni kiashiria cha mazingira huru ya kisiasa, ijapokuwa wasiwasi umeibuliwa kuhusu upendeleo wa vyombo vya habari vya serikali kwa chama tawala cha Zanu PF pamoja na ukosefu wa uwazi katika uchapishaji wa karatasi za kupigia kura.
Serikali ijayo lazima ipambane na ukosefu mkubwa wa ajira na uchumi ulioharibiwa na sera iliyoungwa mkono na Mugabe ya kutwaa mashamba yaliyomilikiwa na wazungu, kuanguka kwa kilimo, kiwango kikubwa cha mfumko wa bei na kuhama kwa wawekezaji.

Mwandishi: rama dee
Mhariri: musa msikiti

Tuesday 15 May 2018

tnt ilitengenezwa mara ya kwanza mwaka 1863

Trinitrotoluene

Trinitrotoluene au kifupi TNT ni kampaundi ya kikemia inayotumiwa hasa kama kilipukaji cha kijeshi.
TNT si kilipukaji kikali zaidi kushinda vingine lakini inapendelewa kwa sababu matumizi yake ni salama kushinda dainamiti au nitrogliserini. Gramu 1 ya TNT inachisha nishati ya jouli 4.184 ilhali gramu 1 ya dainamiti inaachisha jouli 7.500. TNT inayeyuka (kuwa kiowevu) kwenye sentigredi 80 ambayo ni chini ya halijoto yenye hatari ya kulipuka; hivyo inaweza kumwagwa kwa umbo linalotakiwa bila hatari.
Vilevile inavumilia mishtuko na joto bila mlipuko; katika ramia inahitaji mshtuko mkali kwa kusababisha mlipuko. Haiyeyuki kirahisi katika maji kwa hiyo ni salama kwa matumizi katika mazingira nyevunyevu. Tabia hizi zote zilisababisha kuitazamiwa kama kilipukaji salama.

Historia[hariri | hariri chanzo]

TNT ilitengenezwa mara ya kwanza mwaka 1863 na mwanakemia Mjerumani Julius Wilbrand[1] aliyeitumia kama dawa ya rangi njano. Baadaye tabia ya kilipukaji ilitambuliwa lakini haikutumiwa kwa miaka kadhaa kwa sababu vilipukaji kali zaidi kama dainamiti na nitrogliserini zilipendelewa.[2]
Jeshi la Ujerumani lilitambua mnamo 1902 ya kwamba hii ilikuwa faida kwa matumizi ya kijeshi kwa sababu ramia tenye TNT yalikuwa salama zaidi kwa utengenezaji na usafirishaji. Hasa waliona faida ya kwamba ramia ya TNT iliyofyatuliwa na mzinga dhidi ya manowari yenye kinga cha feleji iliweza kutoboa kinga kwanza na kulipuka ndani ya manowari. Hivyo uharibifu wake ulikuwa kubwa zaidi. Waiingereza bado walitumia ramia yenye kilipukaji kali zaidi iliyosababisha mlipuko wakati wa kugonga kinga ya nje na hivyo kuacha nguvu yake nje ya mabnowari. Hivyo Uingereza ulifuata mfano wa Wajerumani tangu 1907 na kujaza ramia zake kwa TNT.
Hadi leo TNT hutumiwa na jeshi za nchi nyingi duniani kwa ajili ya ramia na mabomu. Inatumiwa pia na makampuni ya ujenzi kwa milipuko ya kulengwa wakati wa kubomoa majengo au kuunda nafasi kwenye ujenzi wa barabara.

Tani TNT kama kipimo[hariri | hariri chanzo]

Nguvu ya mlipuko hutajwa kwa kipimo cha "tani ya TNT"; yaani nguvu inayotokea katika mlipuko wa kilogramu 1,000 (= tani 1) za TNT ambayo ni sawa na gigajouli 4.184 [3].
Milipuko mikubwa hasa ya mabomu ya nyuklia hupimwa kwa "kilotani" au "megatani" za TNT. Bomu la nyuklia la kwanza lililotupwa na Marekani huko Hiroshima (Japani) mwaka 1945 lilikuwa na nguvu ya kilotani 15. Mabomu makubwa yaliyotengenezwa wakati wa vita baridi yalikuwa na nguvu zaidi; Marekani iliandaa mabomu hadi megatani 25; mwaka 1961 Umoja wa Kisovyeti (Urusi) ililipusha bomu la nyuklia la jaribio lenye nguvu ya megatani 50 huko kwenye kisiwa Novaya Zemlya.
Hata nishati inayoachishwa wakati wa tetemeko la ardhi inapimwa kwa tani za TNT; tetemeko la ardhi ya 2011 iliyosababisha tsunami nchini Japani imekadiriwa kuwa na nishati ya gigatani 9,320 za TNT , sawa na mara milioni 600 nguvu la bomu la Hiroshima.[4]

Monday 14 May 2018

Watu wafariki kwa ugonjwa wa Ebola DRC

Watu 17 wafariki kwa ugonjwa wa Ebola DRC

Wizara ya afya nchini Congo imethibitisha kuzuka upya kwa ugonjwa wa Ebola, jimboni Equateur kaskazini magharibi mwa nchi hiyo. Visa viwili vya ugonjwa huo, vimethibitshwa baada ya kufanyika kwa uchunguzi.
    
Kongo Ausbruch von Ebola (Getty Images/AFP/D. Minkoh)
Ujumbe wa wataalamu wa afya kutoka serikalini, shirika la afya ulimwenguni na shirika la madaktari wasiokuwa na mipaka unatarajiwa kuwasili baadae siku ya Jumatano kwenye kijiji kilicho athirika na ugonjwa huo.
Wizara ya afya imesema jibu la haraka linahitajika kwa ajili ya kukabiliana na ugonjwa huo ambao kwa sasa umeibuka kwenye kijiji cha Ikoko Impenge, mtaani Bikoro jimboni Equateur. Dr Jean Jacques Muyembe kiongozi wa maabara ya utafiti wa ugonjwa wa Ebola na magonjwa mengine ya kuambukiza amesema kwamba kuna uwezekano mdogo wa ugonjwa huo kusambaa kwenye maeneo mengine
ARCHIV Ebola-Ausbruch in Liberia 2014 (picture alliance/AP Photo/A. Dulleh)
Ebola iliwahi kuripuka nchini Liberia na hapo juu ni wafanyakazi wa afya katika kituo cha ugonjwa huo Monrovia.
"Hatari ya kusambaa kwa ugonjwa huo ni ndogo sana kutokana na kwamba vijiji hivyo vinapatikana kwenye maeneo yasiyofikika kwa urahisi, ni takriban kilomita 200 msituni na mji wa Mbadaka mji mkuu wa jimbo la Equateur. Kwa sababu ugonjwa huo unadhaniwa kuibuka mwezi desemba mwaka jana lakini ni wiki iliopita ndio tumetaarifiwa…Nafiriki ni ugonjwa ambao tunaweza kuutokomeza haraka," amesema Muyembe.
Kwa mujibu wa taarifa ya wizara ya afya ni kwamba kuna visa 21 vya maambukizi ambapo miongoni mwake watu 17 tayari wamefariki, ndio vilisababisha kuweko na tahadhari kuhusu ugonjwa huo. Ujumbe uliopelekwa kwa ajili ya kukadiria tukio ulikuta visa vitano vya watu wenye homa na miongoni mwake watu wawili walikutwa na virusi vya Ebola.
Daktari Muyembe amesema kwamba mtu wa kwanza alihofiwa kufariki kutokana na ugonjwa huo ni afisa wa polisi kwenye kijiji cha Bokatola, ambae alionekana na  dalili za ugonjwa huo . Amesema toka tarehe 3 Mei hakujaripotiwa kifo cha mtu kwenye maeneo hayo.
Ebola-Virus Guinea (picture alliance/AP Photo)
Mripuko wa ugonjwa wa Ebola nchini Guinea
Shirika la Afya ulimwenguni WHO limelezea kwamba liko tayari kuunga mkono juhudi za serikali kwa  ajili ya kuutokomeza ugonjwa huo wa Ebola. WHO imesema imetenga dola milioni moja kwa ajili ya kupambana na ugonjwa wa Ebola jimboni Equateur.
Ni mara ya tisa sasa toka mwaka wa 1976, Congo kutangaza mripuko wa ugonjwa wa Ebola, virusi hivyo vya aina ya zaire vinatokana hasa na ulaji wa nyama mwitu.
Mara ya mwisho ugonjwa huo kuripotiwa nchini humo ilikuwa ni Mei mwaka jana kwenye jimbo la Bas-Uele ambako watu 4 walifariki miongoni mwa visa vinane vilivyothibitishwa.
Hakujakueko na uhusiano wowote baina ya virusi vya Ebola Congo na vile vilivyozuka  mwaka 2014 kwenye nchi za Afrika magharibi vilivyosababisha vifo vya zaidi ya watu 11.

Msichana wa miaka 19 ahukumiwa kifo Sudan

Msichana wa miaka 19 ahukumiwa kifo Sudan

Msichana mmoja aliye na miaka 19 amehukumuhiwa kifo na Korti moja nchini Sudan baada ya kupatikana na hatia ya kumuua mumewe wa kulazimishwa, alipojaribu kumbaka.
    
Indien - Kinderheirat (picture-alliance/AP Photo/P. Hatvalne)
Msichana huyo Noura Hussein alilazimishwa kuolewa na binamu yake akiwa na miaka 16, aliikataa ndoa hiyo na kukimbilia kwa jamaa yake aliyoishi naye kwa miaka mitatu. Baadaye mwezi Aprili mwaka huu alirejea nyumbani nje kidogo ya mji wa Khartoum  baada ya babake kumwambia ndoa hiyo imefutiliwa mbali. Lakini alikuta kuwa mipango ya harusi yake ilikuwa bado inaendelea.
Baada ya kuolewa, Noura alikataa kufanya tendo la ndoa na mumewe na ilipofika siku ya sita, mumewe alimbaka huku jamaa zake wa kiume wakimshikilia Noura kwa nguvu  ili kurahisisha kitendo hicho. Siku ya pili mumewe alijaribu tena kumbaka. Noura alimchoma kisu na kumuua wakati alipojaribu kuzuwia tendo hilo.
Africa Child Marriage Mosambik (picture alliance/AP Photo/S.Mohamed)
Mikono ya msichana aliye na miaka 18 na mumewe wa miaka 20
Aidha Korti ya Sharia inayofuata sheria za kiislamu ilimkuta msichana huyo na kosa la mauaji mwezi uliyopita na siku ya Alhamisi wiki hii, ikamhukumu kifo kwa kunyongwa.
Hata hivyo mawakili wake kwa sasa wana siku 15 za kukata rufaa huku wanaharakati wa kutetea haki za binaadamu wamepaza sauti zao juu ya hili kwa kumtolea wito rais Omar al Bashir kumsamehe msichana huyo,wakisema ilikuwa hatua ya kujilinda. 
"Chini ya sheria ya kiislamu familia ya mume inaweza kudai fidia ya fedha au kifo, walichagua kifo na hicho ndicho kilichofuatwa," alisema  Badr Eldin Salah, mwanaharakati kutoka Vuguvugu la vijana wa Afrika waliokuwa Kortini wakati hukumu hiyo ilipotolewa. 
Badr Salah ameongeza kuwa mawakili wa Noura watakataa rufaa dhidi ya hukumu hiyo lakini pia kunahitajika uungwaji mkono kutoka jamii ya Kimataifa na kutoka katika jumuiya kama Umoja wa Afrika, Umoja wa Mataifa na Umoja wa Ulaya.
Sheria za Sudan zinaruhusu ndoa pindi msichana anapovunja ungo
Sudan imechukua nambari 165 kati ya nchi 188 katika orodha ya Umoja wa Mataifa inayoshughulikia masuala ya usawa wa kijinsia, inayolinganisha nafasi ya  wanawake na wanaume kuhusu upatikanaji wa huduma  za afya, elimu, ujumuishwaji kisiasa na fursa za ajira.
Sudans Präsident Omar Hassan el Bashir, Porträt (dpa)
Rais wa Sudan Omar el Bashir
Sudan ni mojawapo ya nchi barani Afrika zilizo na sera dhaifu kuwalinda wanawake na wasichana. Kwa mfano Ubakaji katika ndoa pamoja na ndoa za utotoni hazichukuliwi kama kosa. Sheria za taifa hilo zinaruhusu msichana kuolewa pindi anapovunja ungo, na zinakubali pia msichana wa miaka kumi kuolewa na mlezi wake kwa ruhusa ya jaji.
Wakati huo huo Yasmeen Hassan Mkurugenzi wa shirika la Equality Now amesema Noura ni mhanga na anapaswa kushughulikiwa kama muathirika, huku akisistiza kuwa katika mataifa mengi muathirika kama Noura hupata huduma mbali mbali ili kuhakikisha anaondokewa na kiwewe baada ya kukutwa na tukio kama hilo.
Yasmeen anasema kumhukumu tu kwa tukio la uhalifu kutokana na kujilinda na shambulio  ni udhalilishaji wa haki zake chini ya katiba ya Sudan na chini ya sheria za kimataifa.
Mwandishi:  rama dee
Mhariri: radick dee david

kundi Alshabaab la ashtakiwa Ujerumani

Mshukiwa wa kundi la Alshabaab ashtakiwa Ujerumani

Waendesha mashtaka wa Ujerumani wamemfungulia mashitaka mwanamume mmoja kutoka Somalia anayedaiwa kuwa mwanachama wa kundi la wanamgambo wa Al Shabab
    
Somalia Al-Shabaab Kämpfer (picture alliance/AP Photo/F. A. Warsameh)
Maafisa nchini Ujerumani wamemfungulia mashitaka mwanamume mmoja kutoka Somalia anayedaiwa kuwa mwanachama wa kundi la waasi la Al Shabab anayetuhumiwa kufanya jaribio la mauaji na kusaidia katika mauaji. Waendesha mashitaka wa Ujerumani wamesema mtuhumiwa huyo mwenye umri wa miaka 20 anayetambulika kwa jina Abduqaadir A alijiunga na kundi hilo la waasi mwaka 2012 mjini Mogadishu na alipewa mafunzo ya kutumia bastola na magureneti.
Wakati wa mafunzo hayo, inadaiwa mshukiwa huyo aliandamana na wanachama wengine wa Al Shabab kwenda msikiti ambako walimuua mtu mmoja kwa kumpiga risasi tatu kichwani. Baadaye aliagizwa kumuua afisa mmoja wa serikali ya Somalia katika mkahawa mmoja. Alifanikiwa kutoroka Somalia mwezi Okotoba mwaka 2012 na alikimbilia Ujerumani mwaka 2014 kabla ya kukamatwa mwezi Februari mwaka huu.

Monday 16 April 2018

Watu 257 wafa kwenye ajali ya ndege Algeria

Watu 257 wafa kwenye ajali ya ndege Algeria

Takriban watu 257 waliokuwa kwenye ndege ya kijeshi nchini Algeria wamefariki dunia baada ya ndege hiyo kuanguka nje ya mji mkuu wa nchi hiyo Algiers. Ndege hiyo iliwaka moto baada ya kuanguka.
Militärflugzeug in Algerien abgestürzt (Reuters/R. Boudina)
Takriban watu 257 waliokuwa kwenye ndege ya kijeshi nchini Algeria wamefariki dunia baada ya ndege hiyo kuanguka nje ya mji mkuu wa nchi hiyo Algiers hii leo. Kulingana na shirika la habari la serikali, ndege hiyo iliwaka moto baada ya kuanguka katika tukio linalotajwa kuwa baya zaidi kwenye usafiri wa anga kuwahi kushuhudiwa nchini humo. 
Picha zilizorushwa na kituo kimoja cha televisheni kinaonyesha watu na magari ya msaada wa dharura wakiwa wamefurika kuzunguka eneo hilo la ajali lililotawaliwa na moshi na moto, karibu na uwanja wa ndege wa kijeshi kwenye kambi ya Boufarik kusinimagharibi mwa Algiers. 
Wizara ya ulinzi imesema, jumla ya watu 257 wamekufa, wengi miongoni mwao ni wanajeshi. Wahudumu 10 wa ndege na baadhi ya abiria waliokufa wamekwishatambuliwa na jamaa zao. Imeongeza kuwa manusura kadhaa wanaendelea kupata matibabu katika hospitali ya jeshi, na miili ya wahanga wa ajali hiyo imepelekwa hospitalini hapo kwa ajili ya utambuzi.
Chanzo cha ajali bado hakijajulikana na tayari kumeanzishwa uchunguzi.
Militärflugzeug in Algerien abgestürzt (Reuters/Ennahar Tv)
Ni tukio la kwanza kwa ndege za jeshi la algeria kutokea tangu mwaka 2014.
Mmoja wa wanachama wa chama tawala cha National Liberation Front, FLN, amekiambia kituo binafsi cha televisheni kwamba miongoni mwa waliokufa ni wanachama wa kikundi cha wanaotaka uhuru wa taifa jirani la Sahara Magharibi, la Polisario, linaloungwa mkono na serikali ya Algeria. Eneo hilo la Sahara Magharibi linazozaniwa kwa muda mrefu na Morocco na Algeria. 
Ni miongoni mwa matukio yaliyowahi kutokea, ingawa hili ni baya zaidi.
Ndege hiyo ilikuwa inaelekea katika mji wa Tindouf, ulioko mpakani mwa Algeria na Sahara Magharibi, lakini ilianguka katika eneo la uwanja wa ndege, hii ikiwa ni kulingana na wizara ya ulinzi. Tindouf ni makazi ya maelfu ya wakimbizi na wengi wakitokea Sahara Magharibi, ambao miongoni mwao ni wafuasi wa Polisario.  
Kulingana na kituo cha televisheni cha Dzair, watu watano wako katika hali mbaya. Mkulima mmoja amekiambia kituo cha televisheni cha Ennahar kwamba aliwaona baadhi ya abiria waliruka kutoka kwenye ndege hiyo kabla ya kuanguka. 
Ofisi ya waziri mkuu imesema wabunge walisimama kimya kwa dakika moja kuwaombea wahanga wa ajali hiyo. 
Ndege hiyo chapa 11-76 iliyoundwa nchini Urusi miaka ya 1970 kwa muda wote imekuwa na rekodi nzuri ya kiusalama. Imekuwa ikitumiwa kwa usafirishaji wa mizigo na abiria. 
Tukio hili ni la kwanza kwa ndege za jeshi la Algeria kutokea, tangu lile la mwezi Februari mwaka 2014, ambapo ndege iliyotengenezwa nchini Marekani chapa C-130 Hercules turboprop ilipoanguka kwenye milima ya Algeria, na kusababisha vifo vya watu 76 na mmoja tu alinusurika.
Tukio baya zaidi la ajali ya ndege kutokea kwenye ardhi ya Algeria ni la mwaka 2003, wakati watu 102 walipokufa na mmoja kunusurika baada ya ndege ya kiraia kuanguka ilipofika mwishoni mwa njia ya kurukia katika uwanja wa Tamanrasset. 

Winnie Mandela hatuta msahau

Winnie Mandela apewa mazishi ya kitaifa

Maelfu ya watu wamekusanyika Jumamosi (14.04.2018) katika uwanja wa mpira wa Soweto kutoa heshima zao za mwisho kwa mwanaharakati wa kupinga ubaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini Winnie Madikizela-Mandela.
Südafrika Bebgräbnis von Winnie Madikizela-Mandela in Johannesburg (Reuters/S. Sibeko)
Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa ametoa heshima yake iliyojawa hisia akiahidi kupendekeza Bi. Winnie apokee heshima ya juu ndani ya chama tawala cha African National Congress ANC. Ramaphosa amemtaja Winnie kama mtu aliyekuwa akijivunia, mtetezi na mwenye kueleza kwa ufasaha aliyefichua uongo wa wabaguzi.
Amesema kuwekwa kizuizini, mateso na miaka ya marufuku ambayo Madikizela-Mandela alipitia, vilimtia hamasa kama mwanaharakati wa kisiasa, lakini pia vilisababisha majeraha makubwa ambayo hayajawahi kupona na kwa kiasi kikubwa kupuuzwa na rika nyingi.
Winnie Madikizela-Mandela aliyefariki Aprili 2, akiwa na umri wa miaka 81 amezikwa kwa heshima ya kitaifa ambapo jeneza lake lilibebwa na askari wakati mwili wake ukiingizwa katika uwanja wa Soweto.
Viongozi kadhaa wa nchi walihudhuria mazishi hayo akiwemo rais wa Congo Brazzaville Denis Sassou Nguesso, waziri mkuu wa taifa jirani la Lesotho Pakalitha Mosisili; na wajumbe wengine kutoka serikali za afrika na vyama vya ukombozi. Marais wa zamani wa Afrika Kusini Jacob Zuma na Thabo Mbeki pia nao walihudhuria mazishi ya mpambanaji huyo aliyejulikana mama wa taifa au mama Winnie.
Mwandishi: Radick Nap Africa
Mhariri: Rama Dee

Wanasiasa wa Urusi wakutana na al-Assad

Wanasiasa wa Urusi wakutana na al-Assad

Wanasiasa wa Urusi wamekutana na Rais wa Syria Bashar al-Assad, siku moja baada ya mashambulizi ya pamoja ya angani ya Marekani, Uingereza na Ufaransa nchini Syria
Syrien Regierungstruppen in Ost-Ghouta (Getty Images/AFP/Y. Karwashan)
Vyombo vya habari vya Urusi vimesema Al-Assad ameusifu mfumo wa enzi ya Kisovieti wa kujikinga dhidi ya makombora ambao Syria inaripotiwa kutumia kuyaripua karibu makombora 70 kati ya 100 yaliyofyatuliwa wakati wa mashambulizi hayo.
Pia ameyaelezea mashambulizi hayo kuwa kitendo cha uchokozi wa nchi za Magharibi, maoni ambayo yameungwa mkono na wabunge hao wa Urusi waliomtembelea.
Kwa mujibu wa shirika la habari la Urusi TASS, Sergei Zheleznyak amesema baada ya mkutano na al-Assad kuwa kutokana na mtazamo wa rais, huu ni uchokozi na tunamuunga mkono.
UN-Sicherheitsrat in New York | Abstimmung Syrien (Reuters/E. Munoz)
Baraza la Usalama lilipinga azimio la Urusi
Warusi hao waliomtembelea wamemuelezea al-Assad kuwa katika "hisia nzuri”. Rais huyo wa Syria pia ameripotiwa kukubali mwaliko wa kuitembelea Siberia, ijapokuwa haijafahamika ni lini ziara hiyo itafanyika. Juammosi, rasimu ya azimio lililowasilishwa na Urusi katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa likiyalaani mashambulizi hayo ya angani halikupitishwa.
Kazi ya OPCW yaanza mjini Douma
Ziara ya wanasiasa hao imefanywa katika siku moja ambayo shirika la habari la Ufaransa – AFP limeripoti kuwa wakaguzi kutoka Shirika la Kimataifa la Kudhibiti Matumizi ya Silaha za Sumu – OPCW wanatarajiwa kuanza uchunguzi wao wa kubaini kama silaha za gesi ya klorini au sarin zilitumiwa dhidi ya raia katika shamubulizi hilo la Aprili 7 mjini Douma.
Wapelelezi hao waliwasili Juammosi, muda mfupi tu baada ya mashmbulizi hayo ya washirika kufanywa. Urusi na Iran ambayo ni mshirika wake anayemuunga mkono Syria ziliyalaani mashambulizi hayo ya angani yaliyoongozwa na Marekani kwa kufanywa kabla ya shirika la OPCW kufanya uchunguzi.
Mkutano wa kilele wa Jumuiya ya Kiarabu kuijadili Syria
Kairo Arabische Liga Außenministertreffen Jerusalemfrage (picture-alliance/Photoshot/A. Gomaa)
Jumuiya ya Kiarabu ilikutana mwisho Machi 2017
Wakati Assad aliwaalika wabunge wa Urusi, viongozi wengine wa mataifa ya Kiarau walikutana nchini Saudi Arabia leo Jumapili kwa mkutano wao wa kilele wa kila mwaka wa Jumuiya ya Kiarabu, ambao ulikuwa umeahirishwa mwezi uliopita kutokana na uchaguzi wa Misri.
Karibu wakuu 17 wa mataifa ya Kiarabu walitarajiwa kuhudhuria mkutano huu mjini Dhaharan. Al-Assad hajashiriki katika mkutano huo wa kilele tangu 2011, wakati shirika hilo lenye nchi 22 wanachama lilipoufuta uwanachama wake.
Ujumbe wa Qatar unaongozwa na mwakilishi wake wa kudumu katika Jumuiya ya Kiarabu, badala ya afisa mwandamizi katika ufalme wa nchi hiyo – ishara kuwa mvutano wa kikanda kati ya Qatar na baadhi ya mairani zake bado ni mkubwa.
Miongoni mwa mada kuu zinazotarajiwa kujadiliwa katika mkutano huo wa kilele ni pamoja na kitu kinachoonekana kuwa ni Iran kuingilia masuala ya nchi za Kiarabu, kama vile vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Yemen na katika kuunga mkono mapigano ya Washia nchini Iraq.
Mashambulizi ya angani nchini Syria mwishoni mwa wiki na vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyodumu miaka saba sasa nchini humo pia ni mambo yanayotarajiwa kujadiliwa.
Mwandishi: Radick nap Africa
Mhariri: Rama Dee