NAP AFRICAN
WORLD CHANGE
Monday 30 July 2018
asili yetu
IDHAA YA KISWAHILI
/
Asili ya Afrika
Nelson Mandela, baba wa demokrasia Afrika
Nelson Mandela ni moja kati ya wapigania uhuru nguli wanaopendwa Afrika. Alitumikia kifungo cha miaka 27 jela, lakini baadae alikuwa ni alama ya mapambano ya kudai uhuru wa nchi hiyo. Alisaidia kuiongoza nchi yake, kutoka kwenye siasa za ubaguzi wa rangi kuwa za kidemokrasia, na baadaye kuwa Rais wa kwanza mweusi wa Afrika ya kusini. Anakumbukwa kama mfano wa kuigwa, unyenyekevu, na huruma zake.
Kutana na Siti binti Saad
Siti Binti Saad kutoka kisiwa cha Unguja, Zanzibar, aliivunja miko ya Taarab na akawa mwanamke wa kwanza ambaye hajasoma kuimba mtindo huo wa muziki kwa Lugha ya Kiswahili.
Mfahamu Patrice Lumumba
Unamfahamu kwa kiasi gani Patrice Lumumba? Tunamuangazia mwanaharakati huyo aliyekuwa maarufu na hadi leo jina lake limezidi kuwa maarufu.
Tazama vidio
01:50
Mfahamu mfalme Haile Selassie wa Ethiopia
Jua historia ya Haile Selassie Mwanamfalme kijana RasTafari Makonnen aliyevikwa taji la mfalme Haile Selassie mwaka 1930.
Vidio zaidi
Ngungunyane: mfalme dhidi ya utawala wa Kireno
Malkia Muhumuza - aliyepambana na ukoloni
Mwanamapinduzi Thomas Sankara
Njinga Mbande - Shujaa wa kidiplomasia
Mtambue Sundiata Keita
Yaa Nana Asantewaa - Malkia wa vita
Mfahamu mfalme Haile Selassie wa Ethiopia
Kutana na Josina Machel mpigania uhuru wa Msumbiji
Josina Machel ni mwanamke aliethubutu kuinua silaha dhidi ya utawala wa kikoloni wa Kireno. Aliwahamasisha wanawake wengine pamoja na wanaume kuingia vitani kudai uhuru katika eneo lijulikanalo sasa kama Msumbiji.
Mjue shujaa wa Namibia Hendrik Witbooi
Hendrik Witbooi ni shujaa anaeheshimiwa nchini Namibia kwa kuliongoza kundi la watu walioitwa Nama kupigana na Wakoloni wa Ujerumani.
Charlotte Maxeke, alipambana haswa na ubaguzi wa rangi
Kutana na Charlotte Maxeke, mwanamke wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini kuhitimu chuo kikuu. Aliwaongoza wanawake katika maandamano dhidi ya matabaka. Baadae alianzisha chama cha kwanza cha wanawake nchini Afrika Kusini. Fuatilia historia yake katika mfululizo wa Makala za Asili ya Afrika.
Tazama vidio
01:23
Kutana na Malkia wa Sheba
Malkia wa Sheba ambaye pia anajulikana Makeda ni kitovu cha mithiolojia nchini Ethiopia.
Vidio zaidi
Kutana na Malkia wa Sheba
Bayajida - baba wa kabila la Hausa
Mtambue Dinknesh
Kutana na Mwalimu Julius Nyerere
Kutana na Cheikh Diop, mwanasayansi wa Kiafrika
Mjue Kinjekitile Ngwale
Unamfahamu Kwame Nkrumah?
Umesikia nini kumhusu Ahmed Baba
Timbuktu uliposhambuliwa, na kudhibitiwa na Sultani wa Morocco, Ahmed Baba alipelekwa Marrakesh ambapo aliruhusiwa kufundisha na kuandika. Ametunga zaidi ya vitabu 50.
Mwanasiasa wa kwanza wa kike Nigeria, Margaret Ekpo.
Mwanaharakati huyo wa kike na mwanasiasa Nigeria, Margaret Ekpo alisaidia kubadilisha sura ya siasa za Nigeria. Alikuwa mwenye nguvu. Alikuwa mzungumzaji. Aliwapa wanawake msukumo. Hii hapa hadithi yake
Kutana na Mwanamfalme Louis Rwagasore
Mwanamfalme Louis Rwagasore ni miongoni mwa watu waliopigania uhuru barani Afrika na ambao hawajulikani sana. Alifanikiwa kuiongoza Burundi hadi uhuru kwa njia ya amani.
Kutana na Sarah Baartman
Kutana na Sarah Baartman kutoka mjini Cape Town Afrika Kusini mwaka 1810. Mwanamke mdogo wa Khoikhoi aliyefanya kazi katika nyumba ya "mtu huru mweusi". Alitumikishwa kama mnyama na kuwa muhanga wa ubaguzi wa kisayansi. Alikufa akiwa maskini katika umri wa miaka 55. Kwa zaidi ya karne wageni wa makumbusho ya taifa ya Ufaransa, waliutizama ubongo wake, mifupa na viungo vya uzazi.
Mjue Amilcar Cabral na vuguvugu la ukombozi wa Guinea Bissau na Cape Verde
Akiibuka kutoka kundi la wapigania uhuru wa Afrika, Amilcar Cabral ameiongoza Guinee Bissau na Cape Verde kuelekea uhuru kutoka watawala wa kikoloni wa Ureno. Lakini aliuliwa kabla ya kulifikia lengo lake.
No comments:
Post a Comment
Newer Post
Older Post
Home
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment