Mawe yaliyochongwa kuwa na
kona kali kwa matumizi kama
kisu.
Mtu wa zama za mawe akikata
mti.
Utamaduni wa watu kwenye chanzo cha zama za mawe
Lakini
meno na ma
kucha yake hayafai kupasua ngozi ya mnyama mkubwa au kukata
nyama yake vipande-vipande akitaka kubeba windo hadi mahali penye
familia yake. Vilevile makucha hayafai sana kuchimba mizizi kwa chakula.
Hapo binadamu aliweza kutumia vitu vinavyopatikana kiasili katika
mazingira: jiwe lenye kona kali,
tawi la mti lenye
ncha kali pamoja na vipande vya
mifupa. Hivyo vyote vilisaidia shughuli za kuchimba, kupasua na kukata.
[1]
Kuna
mabaki mengi ya mawe yaliyochongwa kwa matumizi kama vifaa na mabaki hayo yamekuwa msingi wa jina "zama za mawe". Vifaa hivyo na
mabadiliko yake vinaonyesha
maendeleo katika
maisha ya binadamu na kuongezeka kwa uwezo wake wa kupambana na mazingira yake.
Kwa hiyo ni kipindi cha matumizi ya mawe yaliyochongwa kuwa vifaa baada ya kipindi ambako watu walitumia fimbo tu au mawe katika hali asilia na kabla ya kipindi ambapo watu walielewa namna ya kutumia
metali.
Kifaa cha mawe sahili - zama za mawe ya kale
Shoka la mkononi - bapa pande mbili (mwishoni mwa Zama za mawe ya kale) - inaonyeshwa kutoka mitazamo mbalimbali
Vipindi vya zama za mawe
Wataalamu wa
akiolojia wametambua ya kwamba vifaa vya mawe vinaonyesha tabia tofautitofauti.
- Kuna vifaa sahili sana kama jiwe lililogongwa mara moja ili kipande kivunjike na ncha kali ipatikane.
- Kuna pia vifaa vya mawe vinavyoonyesha maendeleo zaidi; vilifanyiwa kazi kwa siku kadhaa kiangalifu ili kunyoshwa, kung'arishwa na kutobolewa kwa kuweka pini.
Kutokana na tofauti kubwa katika hali ya vifaa vya mawe wataalamu wanaona ya kwamba wanaonyesha
historia ndefu ya maendeleo ya
teknolojia ya kushughulikia jiwe ambako watu walianza kwa vifaa sahili na kuendelea kujifunza zaidi na kuboresha matokeo ya
juhudi zao.
Kwa hiyo wataalamu wengi wanatofautisha:
Si tofauti katika
ubora wa vifaa pekee, lakini kuna pia
dalili nyingine zinazoonyesha ya kwamba watu walibadilisha maisha yao, namna ya kujipatia chakula na makazi.
Kila mtu aliweza kugonga jiwe dhidi ya jiwe hadi ncha kali ilipatikana. Lakini ma
shoka ya mawe yaliyohitaji siku za kazi makinifu yanaonyesha kuwepo kwa
jamii iliyokuwa na ma
fundi wa pekee walioweza kunyosha
ufundi wao wakilishwa na wengine ni pia dalili ya
biashara iliyofanywa hasa tukikuta vifaa vya jiwe fulani katika maeneo ambako jiwe hili halipatikani kiasili.
Pamoja na matokeo mengine ya
utafiti wa akolojia, kama vile mabaki ya ma
kaburi, vyombo vya
ufinyanzi,
nyumba na vifaa vingine, wataalamu waliweza kupata picha ya undani zaidi kuhusu maisha na jamii ya watu wa zamani zile.
Teknolojia ya kupunguza jiwe hadi kupata kisu chembamba - zama za mawe ya kati (Levallois)
Matumizi ya ncha ya jiwe kwenye mkuki
Vifaa vya mawe
Zama za mawe ya kale
Vifaa vya kwanza vilikuwa mawe yaliyokatwa upande mmoja ili kuwa na kona kali moja. Hatuwezi kujua kwa uhakika tukiona jiwe la aina hii kama kama ilikuwa tokeo la mgongano wa mawe katika mkondo wa maji mtoni au kutokana na kuanguka kwa jiwe kutoka mlimani au kama jiwe limepigwa kwa kusudi kwa jiwe lingine kwa shabaha ya kupata kona kali. Lakini mawe haya yalifaa kutumiwa kwa kukata pia si vigumu kuvitengeneza.
Mifano ya kale kabisa ya mawe yaliyogongwa kwa mawe mengine kwa kusudi la kupata kona kali zimepatikana katika eneo la
ziwa Turkana (leo nchini
Kenya) yalitegenezwa miaka milioni 3.3 iliyopita
[2].
Ngazi iliyofuata ni mawe yaliyofanyiwa kazi zaidi hadi kuwa "shoka la mkononi". Hapo jiwe la kufaa lilipigwa na kupunguzwa pande zote mbili hadi kuwa na bapa pande mbili. Sehemu ya juu ilibaki bila ukali kwa kuishikilia mkononi. Kuna mahali ambako mabaki mengi ya mashoka haya ya mkononi yamepatikana katika hali mbalimbali: mawe yaliyopigwa kiasi, mawe yaliyovunjika vibaya na kutupwa, vipande vidogo vilivyopasuliwa wakati wa kuipa shoka umbo lake na kadhalika. Mahali pale panatazamwa kama
karakana au viwanda vya kutengeneza vifaa vya mawe. Mahali mashuhuri katika
Afrika ya Mashariki ni
bonde la
Isimila(karibu na
Iringa,
Tanzania ya leo).
Zama za mawe ya kati
Kipindi hiki kinatazamwa kilianza miaka 300,000 iliyopita na kudumu hadi miaka 25,000 - 50,000
[3] iliyopita.
Mabamba makali ya mawe yamefungwa katika ubao wa mundu ya kukatia majani au mazao
Kipindi hiki kinaonyesha maendeleo ya teknolojia. Watu walianza kutumia pia vipande vidogo vikali vilivyopatikana wakati wa kupunguza jiwe. Vibanzi vikali vya mawe vilifungwa sasa kwenye pini ya ubao kwa gundi la miti. Kwa njia hii vifaa kama
kisu,
chusa au
mundu vilipatikana.
[4]
Matatizo ya lugha ya "zama za mawe"
Zama za mawe zilikuwa vipindi virefu sana cha miaka elfu nyingi. Wataalamu wamegawanya zama hizi kwa vipindi mbalimbali kama Zama za mawe za kale na Zama za mawe za kati. Tofauti hizi zinaonekana kutokana na lakini wataalamu wa siku hizi wanaona ya kwamba mgawanyo huu ulitazama zaidi
historia ya Ulaya isiyolingana na historia ya sehemu nyingine za
dunia.
Tatizo kuu la mafundisho ni ya kwamba ni kipindi cha teknolojia bila kuangalia pande nyingine za maendeleo ya kibinadamu.
Hata hivyo lugha ya "zama za mawe" imekuwa kawaida duniani na wataalamu wanaendelea kuitumia wakijua
kasoro zake kwa sababu hadi hasa hakuna mawazo ya kufaa zaidi.
Kifaa cha jiwe - awamu ya kwanza
-
Shoka la mkononi hali ya juu - kutoka Ethiopia
Matumizi ya shoka la mkononi
Mashoka ya mawe yaliyonyoshwa - awamu za baadaye
Shoka la mawe lenye shimo la pini
No comments:
Post a Comment